Translate

Monday, June 6, 2016

Intent to Fast - Kutia Niya ya Kufunga

What to say when you intend to make fast.
Chakusema wakati unataka kutia niya ya kufunga.

Dua - Intent to keep fast
Natia Nia ya kufunga kesho kwa Mwezi wa Ramadhani.
Jinsi ya kuisema. 
How to say it properly.

Makkah Live HD

Yaani hizi technology, kweli Mwenyezi Mungu ni Mkubwa. Haya Ukishindwa kwenda msikitini kuswali taraweh, live from Makka. Yaani unaswali na masheikh wakumbwa kabisa ukiwa nyumbani.

99 Beautiful Names - Spoken Word by Boonaa Mohammed

Let's Kick off this Ramadhan right! Happy fasting folks 2016, you can absolutely do it. If you couldn't fast in the past, now is your chance to start. Let's get those blessings going, outweigh your sins with good, oh and don't forget to give back to your communities.
Bismillah!

Sunday, June 5, 2016

Muhammad Ali 1942-2016


Cassius Marcellus Clay, Jr.  Almaaruf Muhammad Ali  alizaliwa January 17, 1942 Lousiville, Kentucky Marekani. Alikuwa ni bondia, mpiganaji wa haki za mwananchi na za kibanadamu na Mtu wa dini.


Ali katoka kwenye familia ya watoto watano, dada moja na kaka zake wanne. Alikuwa ni bondia maarufu wa kimarekani, na alishinda Olympic Gold Medal akiwa na miaka 18. Akiwa na miaka 22 alishinda mashindano ya ubondia wa dunia mwaka 1964. Baada ya hapo alibadilisha dini na Jina akaitwa Muhammad Ali. Mwaka 1966, Ali aligoma kwenda kupigana kwenye vita vya vietnam, kitendo ambacho kilimfanya afungwe jela, na kunyanganywa pasipoti yake, na medali zake za ushindi. Mwaka 1971, alirudisha kesi yake kotini na akashinda.

Ali aliendelea kushindana kwenye ubondia, na akatoka mshindi mwaka 1974 na 1978 akapewa jina la the greatest kwasababu ya kushinda ubondia wa dunia mara tatu. Ali, alistaafu ubondia mwaka 1981. Mwaka 1984 Ali tambuliwa na ugonjwa wa Parkinsons, ni ugonjwa ambao wakati mwingine unakuja kwa ajili ya kichwa kupigizwa na kuna uwezekano aliupata kutokana na kazi yake.

Mwaka 1991 kwenye Golf War, Ali alienda Iraq kukutana na Sadam Hussein kuongea nae ili awaachie mateka wa kimarekani. Mwaka 2002, Alienda Kabul, Afghanistan kama Mjumbe wa Amani wa Umoja wa Mataifa. Mwaka 2001 alipewa medali ya Presidential Citizens Medal na Raisi Clinton, na mwaka 2005 alipewa Presidential Medal of Freedom na Raisi Bush. Mwaka 2007 center ya Muhammad Ali ilifunguliwa kwenye mji wa Lousville, Kentucky.

Muhammad Ali alifariki na Septic Shock, baada ya kulazwa hospitalini siku tano kwa matatizo ya pumzi, kaacha Mke na watoto nane.

Mwenyezi Mungu amuwekee Nuru kwenye Kaburi lake, na ampokee kwenye pepo yake.

He was God Fearing and Made sure we knew about it, every chance he got.

Ramadhan 2016 Starts on Monday June 6th

Hurray! We start fasting tomorrow on Monday the 6th, so tighten those belts and let's do it right this time.  The moon sighting committee of UAE and Saudi have announced the moon was sighted in the region on Sunday June 5th. The Fiqh council of North America have also announced Ramadhan to start tomorrow. Let's wipe out our sins on the first 10 days of mercy in'shaa'llah.

Mwezi umeonekana uarabuni na wametangaza Ramadhani unaanza kesho Jumatatu Juni 6. Fiqh council ya Marekani pia wametangaza mwezi wa ramadhani kuanza kesho. Na nimesikiliza Radio Ihsan, Mwenyekiti wa  Baraza la wana Sunna Tanzania akitangaza Ramadhani kuanza Kesho, Kutokana na taarifa za Mwezi kuonekana sehemu mbali mbali ikiwemo handeni Tanga. Kwa hiyo wandugu tunaanza kufunga kesho, tujitahidi tufanye mema ili madhambi yetu yafutwe kati ya siku kumi hizi za mwanzo za msamaha.

Mwenyezi Mungu akubali funga zetu, akubali sala zetu, atusamehe madhambi yetu na atulinde na mabaya ya hii dunio, adhabu ya kaburi na moto wa Jahaman.

May Allah forgive Accept our fast, accept our prayers, forgive our sins and protect us from the bad of this world and the fire of hell .


Update!
Nimepata Habari Sheikh Jongo Kadhi wa Dar Es Salaam katangaza kwenye Radio Kheri kwamba Ramadhani inaanza Jumanne. Haya Ramadhani Njema kwa ndugu zangu watakao anza Jumatatu na wale pia watakao anza Jumanne. In'Shaa'llah Mwenyezi Mungu atufanyie wepesi.

Happy Ramadhan to everyone starting on Monday and also those folks starting on Tuesday.

Thursday, June 2, 2016

Amulets - Hirizi

Haya mkayatupe kabisa yale ma kinga, toa yale mavisu na ndimu kwenye vitanda vya watoto, na yale ma hirizi na vitanzi. Usiweweseke, Allah Peke yake ndio kinga yako.