Translate

Thursday, May 1, 2014

Watu 19 wauliwa Singida

Jamani hizi habari zinasikitisha. Hawa waendesha mabasi wetu wako rough sana.  Kwanini ukiona umati wa watu pembeni ya barabara, obviously wana clear accident scene, hupunguzi mwendo? Muendesha basi kweli ni wa kulaumiwa, kwasababu hakuweza kufikiria fasta fasta, jinsi ya kukwepa hilo gari lilokua linakuja kutoka upande mwingine wakati wanalipita gari la polisi. Its understandable as he was in a state of panic. Je huyo aliyosababisha hiyo confusion, na yeye anamakosa? What about hao polisi wenyewe, kama walikuwa wana clear an accident scene, yako wapi yale ma triangle mekundu ambayo wanatusimamisha kutwa barabarani kutukagua kama tunayo? Je kwanini hakukuwa na polisi moja pia wa ku control flow ya traffic? What about hiyo barabara ilivyo undwa hapo, je design yake inahitaji kupitiwa tena? Kwakweli, maswali ni mengi, walio changia haya makosa ni wengi na lawama ni nyingi. Tunahitaji ku revisit sheria zetu za barabarani, madereva wetu wote wanabidi wawe retrained jinsi ya kuendesha gari barabarani. I hope haki itatendeka, na wenye makosa watakuwa held responsible.

Inna lillahi Waina Illahi Raji'un
Kwa Mwenyezi ndio tunapotoka na ndio marejeo.
Nawaombea Allah awapokee waliofarika kwenye pepo yake, na awaliwaze familia za marehemu.

Nenda EATV usome mkasa wote wa hii ajali.



No comments:

Post a Comment