Translate

Friday, June 26, 2015

Aya za Leo - Hadithi ya Lut (The Story of Lut)

Lut'i akamuamini, na akasema: Mimi nahamia kwa Mola wangu Mlezi. Hakika Yeye ndiye Mwenye nguvu, Mwenye hikima.Na pale Lut'i alipo waambia watu wake: Hakika nyinyi mnafanya uchafu, ambao hapana mmoja katika walimwengu aliye kutangulieni kwa hayo.
Je! Nyinyi mnawaingilia wanaume, na mnaikata njia? Na katika mikutano yenu mnafanya maovu? Basi haikuwa jawabu ya watu wake isipo kuwa kusema: Tuletee hiyo adhabu ya Mwenyezi Mungu ikiwa wewe ni katika wasemao kweli.Akasema: Ewe Mola wangu Mlezi! Ninusuru na watu mafisadi hawa! Na wajumbe wetu walipo mjia Ibrahim na bishara, walisema: Hakika sisi hapana shaka tutawahiliki watu wa mji huu, kwani watu wake hakika wamekuwa madhaalimu.Akasema: Hakika humo yumo Lut'i. Wao wakasema: Sisi tunajua zaidi nani yumo humo. Hapana shaka tutamwokoa yeye na ahali zake, isipo kuwa mkewe aliye miongoni mwa watao kaa nyuma. Na wajumbe wetu walipo mfikia Lut'i, alihuzunika kwa ajili yao, na moyo uliona dhiki kwa ajili yao. Wakasema: Usiogope, wala usihuzunike. Hakika sisi tutakuokoa wewe na ahali zako, ila mkeo aliye miongoni mwa watao kaa nyuma.Kwa yakini sisi tutawateremshia watu wa mji huu adhabu kutoka mbinguni kwa sababu ya uchafu wanao ufanya.Na tumeacha katika mji huo Ishara ilio wazi kwa watu wanao tumia akili zao.

But Lut had faith in Him: He said: "I will leave home for the sake of my Lord: for He is Exalted in Might, and Wise." And (remember) Lut: behold, he said to his people: "Ye do commit lewdness, such as no people in Creation (ever) committed before you.
"Do ye indeed approach men, and cut off the highway?- and practise wickedness (even) in your councils?" But his people gave no answer but this: they said: "Bring us the Wrath of Allah if thou tellest the truth."He said: "O my Lord! help Thou me against people who do mischief!"When Our Messengers came to Abraham with the good news(his wife getting a baby), they said: "We are indeed going to destroy the people of this township: for truly they are (addicted to) crime." He said: "But there is Lut there." They said: "Well do we know who is there : we will certainly save him and his following,- except his wife: she is of those who lag behind!".And when Our Messengers came to Lut, he was grieved on their account, and felt himself powerless (to protect) them: but they said: "Fear thou not, nor grieve: we are (here) to save thee and thy following, except thy wife: she is of those who lag behind."For we are going to bring down on the people of this township a Punishment from heaven, because they have been wickedly rebellious."And We have left thereof an evident Sign, for any people who (care to) understand.
(Qur'an 29:26,28-35)
Ijumaa Njema Wadau!



Thursday, June 25, 2015

Wednesday, June 24, 2015

Mawaidha ya Leo kutoka kwa Sheikh Nurdin Kishki

Shk.Nurdin Kishki, Tumechukua Tabiya Za Wasiokuwa Waisilamu. (2015)

Ukitaka kujua historia yake, mcheki post yangu ya nyuma ya Msomi wa Leo hapa>>>>

Monday, June 22, 2015

Aya za Leo - The Story of Ibrahim Part 2(The Dialogue)



(Qur'an 26:69-104)
Na Wasomee habari za Ibrahimu. 
Alipomwambia baba yake na kaumu yake, "mnaabudu nini?"
Wakasema, "Tunaabudu masanamu, daima tunawaabudu."
Akasema, "Je, yanakusikieni mnapoyaita? Au yanakufaeni (mkiyaabudu) au yanakudhuruni (Mkiacha kuyaabudu)?
Wakasema, "Hayafanyi haya lakini tumewakuta baba zetu wakifanya hivi."
Akasema, "Je, mumewaona hawa mnaowaabudu nyinyi na wazee wenu waliotangulia? Bila shaka hao ni adui zangu ila Mola wa walimwengu wote, ambaye ameniumba na yeye ndio ananiongoza. Na ambaye ndiye anayenilisha na kuninywesha. Na ninapougua, yeye ndiye anayeniponesha. Na ambaye atanifisha kisha atanihuisha.Na ndiye ninayemtumaini kwamba atanisamehe makosa yangu siku ya malipo.

Mola wangu! nipe hukumu na uniunge pamoja na watendao mema. Na unijaalie katika warithi wa mabustani ya neema. Na umsamehe baba yangu, bila shaka yeye ni miongoni mwa waliopotea. Wala usinifedheheshe siku watakayofufuliwa, siku ambayo hayatafaa mali wala watoto.

Isipokuwa mwenye kuja kwa Mwenyezi Mungu na moyo safi, na pepo itasogezwa kwa wacha Mungu, na Jahanamu itadhihirishwa kwa wapotofu.

Na wataambiwa, "wapo wapi mliokuwa mkiwaabudu? Badala ya Mwenyezi Mungu! Je, wanaweza kukusaidieni au kujisaidia wenyewe? Basi watatupwa humo wao na maasi, na majeshi ya Ibilisi yote. Watasema, 'na hali ya kuwa wanagombana humo, 'Wallahi, kwa yakini tulikuwa katika upotofu ulio dhahiri. Tulipokuwa tukikufanyeni sawa na Mola wa walimwengu wote.'

Na hawatakupoteza ila wale waovu.
 'Basi hatuna waombezi wala rafiki halisi. Laiti kama tungelikuwa na marejeo tungekuwa waumini.'"

Bila shaka pana katika haya mazingatio, lakini wengi katika wao si wenye kuamini. Na kwa yakini Mola wako ndiye Mwenye nguvu, Mwenye rehema.

Sunday, June 21, 2015

Tumsifie Na Kumkumbuka Allah kila siku In'Shaa'llah

daily tasbih for ramduhn(english & arabic subtitles)

Aya ya Leo - Ayatul Kursi

Hii Aya waislamu tunashauriwa kuisoma kila siku, ukiisoma usiku, Allah anakuteulia mlinzi kukulinda usiku kucha na mabaya yote mpaka asubuhi. Na asubuhi pia ukiisoma, unapewa mlinzi wakukulinda mpaka usiku.

Mtume Muhammad(S.A.W) alisema, " Yule mwenye kuisoma hii aya baada ya kila sala, basi kifo ndo kinachomzuia yeye kuingia peponi."

Basi tujitahidi kuihifadhi hii aya.
 Ayatul Kursi - Miracles of Quran - Ustadh Nouman Ali Khan
 1. Mwenyezi Mungu - hapana mungu ila Yeye Aliye
hai.Msimamia mambo yote milele. 
2. Hashikwi na usingizi wala kulala. 
3.Ni vyake pekee vyote viliomo mbinguni na duniani. 
4.Ni nani huyo awezaye
kuombea mbele yake bila ya idhini yake? 
5.Anayajua yaliyo mbele yao na
yaliyo nyuma yao.
6. wala wao hawajui chochote katika vilio katika ujuzi
wake, ila kwa atakalo mwenyewe. 
7.Enzi yake imetanda mbinguni na duniani; 
8.Na wala haemewi na kuvilinda hivyo. 
9.Na Yeye ndiye aliye juu, na ndiye
Mkuu
(Qur'an 2:255)

Saturday, June 20, 2015

FUTARIIIII - MATUNDAAAA!!!!!

Ushanunua matunda ya Kufungulia?
 Mara ya mwisho umeenda sokoni mwenyewe kuchagua matunda lini?
Si mnajua lakini matunda hujenga mwili?
 Au teseme inasukuma vitu tumboni, wanasemaga magonjwa yote yanaanziaga kwenye utumbo.

Haya Futari njema wadau, ma fruit salad kwa wingi basi.