Translate

Monday, June 29, 2015

Vitu 8 vya kukusaidia kupata choo



Kuna kuwaga na malalamiko mengi mwezi Ramadhani kutoka kwa watu kuwa hawapati choo. Misemo kama, yaani siku ya nne leo sijapata choo, ni kawaida mno, na ata ukipata ni magumu mno. Wengine hulaumi kwasababu ya kushinda na njaa siku nzima, wengine hutumia hicho kama kisingizio cha kuto kufunga kabisa. Basi isiwe tabu, post ya leo nawapa vitu 8 vya kukusaidia upate choo laini.

1. Maji
Kama ile picha ya juu inavyo elezea, choo kigumu kinatokana na kutokua na maji ya kutosha ili choo kilainike. Time ya kufungua, piga glass zako mbili  za haraka, alafu kunywa maji usiku mpaka ufikishe angalau lita mbili au glasi nane.

2. Matundaa

Matunda yana Fiber ambayo, yenyewe haina virutubisho, lakini kazi yake maalum ni kusukuma chakula tumboni ili kiweze kutoka haraka. Ni vizuri ukiyala kwenye tumbo ambalo halina chakula, yaani kula matunda kwanza kabla ya mlo mwingine. Alafu subiri kidogo kwa muda wa kama lisaa hivi ili chakula kisagike. Kuna Sababu Mtume alikuwa anafungua na Tende na Maji jamani, sio mkate na asali, formula tunayo ni juu yetu kuitumia sawa.
3. Mboga
Mboga za aina yote, ni nzuri kwasababu kama matunda, zina fiber nyingi. Kama kwenu watu hawapendi mboga za majani, then zidisha kachumbari ui serve kama side dish na yenyewe. Biringanya, bamia na kadhalika, ata viazi pia ni mboga.

4.Kunde
Maharage, Njegere, choroko, dengu na kadhalika. Kiufupi kunde za aina yote, hakikisha futari yako haikosi aina moja hapo juu. Nazo zina fiber nyingi mno, na mambo yako yatakuwa swafi.

5.Maziwa ya Mgando
Si kama ice cream hiyo jamani. Maziwa mgando yana vijidudu vizuri ambayo digestive system yetu inahitaji kutusaidia kusaga chakula. Hii pia ule kwenye tumbo ambalo halina chakula, vizuri kufungulia nayo pia.

6. Zoezi
Mazoezi husaidia kuamsha mwili mzima ikiwemo na utumbo wako. Fanya mazoezi pia kwa afya yako.

7. Mafuta ya Zeituni
Kama umefanya 1-6 na vikagoma, basi kunywa kijiko kimoja cha mafuta ya Zeituni, na kijiko kimoja cha ndimu kwenye tumbo tupu.

8. Castor Oil
Hii ni kiboko inasafisha utumbo mzima. Kunywa kijiko kimoja cha chai kwenye tumbo tupu. Mama yangu aliniambia ndio dawa waliyokuwa wanapewa na wazazi wao kusafisha tumbo. Sema hakikisha unanua ambayo ni asilimia 100 castor oil, na cold pressed(mafuta mabichi) ndio mazuri zaidi. Zina patikana kwenye maduka ya dawa.

Zipe muda hizi nilizoziweka hapo juu kufanya kazi, yaani usitegemea utapata choo baada ya lisaa limoja, labda kesho yake, kua mwenye subira kidogo. Kama siku ya pili baada ya kujaribu ya hapo juu mambo bado, basi nenda duka la dawa upate dawa kali zaidi ya kukusadia.

 Swaumu Njema jamani!

Sunday, June 28, 2015

Fungo 10 za mwanzo za Mwezi wa Ramadhani

Salaam aleykum ndugu zangu. Tumemaliza fungo kumi la Mwanzo, vipi mnajisikiaje na swaum? Mie siku ya pili ilinitandika sana. Kwavile tunatambua huu mwezi ni wa toba, na tumemaliza fungo kumi za mwanzo za rehema, na tumesha anza fungo kumi za pili, tujitahidi basi na speed ile ile. Tuhakikishe swala tano tunaziswali na taraweh tujitahidi kwenda, na usiku pia ukiweza amka uswali. Tuendelee kumlilia Allah Shida zetu na kumuomba sana atusamehe madhambi yetu.

Haya nawaacha na Maher Zain anawasadia na maneno ya kumuomba Allah msamaha.

Maher Zain - Forgive Me | Vocals Only (Lyrics)

Friday, June 26, 2015

Aya za Leo - Hadithi ya Lut (The Story of Lut)

Lut'i akamuamini, na akasema: Mimi nahamia kwa Mola wangu Mlezi. Hakika Yeye ndiye Mwenye nguvu, Mwenye hikima.Na pale Lut'i alipo waambia watu wake: Hakika nyinyi mnafanya uchafu, ambao hapana mmoja katika walimwengu aliye kutangulieni kwa hayo.
Je! Nyinyi mnawaingilia wanaume, na mnaikata njia? Na katika mikutano yenu mnafanya maovu? Basi haikuwa jawabu ya watu wake isipo kuwa kusema: Tuletee hiyo adhabu ya Mwenyezi Mungu ikiwa wewe ni katika wasemao kweli.Akasema: Ewe Mola wangu Mlezi! Ninusuru na watu mafisadi hawa! Na wajumbe wetu walipo mjia Ibrahim na bishara, walisema: Hakika sisi hapana shaka tutawahiliki watu wa mji huu, kwani watu wake hakika wamekuwa madhaalimu.Akasema: Hakika humo yumo Lut'i. Wao wakasema: Sisi tunajua zaidi nani yumo humo. Hapana shaka tutamwokoa yeye na ahali zake, isipo kuwa mkewe aliye miongoni mwa watao kaa nyuma. Na wajumbe wetu walipo mfikia Lut'i, alihuzunika kwa ajili yao, na moyo uliona dhiki kwa ajili yao. Wakasema: Usiogope, wala usihuzunike. Hakika sisi tutakuokoa wewe na ahali zako, ila mkeo aliye miongoni mwa watao kaa nyuma.Kwa yakini sisi tutawateremshia watu wa mji huu adhabu kutoka mbinguni kwa sababu ya uchafu wanao ufanya.Na tumeacha katika mji huo Ishara ilio wazi kwa watu wanao tumia akili zao.

But Lut had faith in Him: He said: "I will leave home for the sake of my Lord: for He is Exalted in Might, and Wise." And (remember) Lut: behold, he said to his people: "Ye do commit lewdness, such as no people in Creation (ever) committed before you.
"Do ye indeed approach men, and cut off the highway?- and practise wickedness (even) in your councils?" But his people gave no answer but this: they said: "Bring us the Wrath of Allah if thou tellest the truth."He said: "O my Lord! help Thou me against people who do mischief!"When Our Messengers came to Abraham with the good news(his wife getting a baby), they said: "We are indeed going to destroy the people of this township: for truly they are (addicted to) crime." He said: "But there is Lut there." They said: "Well do we know who is there : we will certainly save him and his following,- except his wife: she is of those who lag behind!".And when Our Messengers came to Lut, he was grieved on their account, and felt himself powerless (to protect) them: but they said: "Fear thou not, nor grieve: we are (here) to save thee and thy following, except thy wife: she is of those who lag behind."For we are going to bring down on the people of this township a Punishment from heaven, because they have been wickedly rebellious."And We have left thereof an evident Sign, for any people who (care to) understand.
(Qur'an 29:26,28-35)
Ijumaa Njema Wadau!



Thursday, June 25, 2015

Wednesday, June 24, 2015

Mawaidha ya Leo kutoka kwa Sheikh Nurdin Kishki

Shk.Nurdin Kishki, Tumechukua Tabiya Za Wasiokuwa Waisilamu. (2015)

Ukitaka kujua historia yake, mcheki post yangu ya nyuma ya Msomi wa Leo hapa>>>>

Monday, June 22, 2015

Aya za Leo - The Story of Ibrahim Part 2(The Dialogue)



(Qur'an 26:69-104)
Na Wasomee habari za Ibrahimu. 
Alipomwambia baba yake na kaumu yake, "mnaabudu nini?"
Wakasema, "Tunaabudu masanamu, daima tunawaabudu."
Akasema, "Je, yanakusikieni mnapoyaita? Au yanakufaeni (mkiyaabudu) au yanakudhuruni (Mkiacha kuyaabudu)?
Wakasema, "Hayafanyi haya lakini tumewakuta baba zetu wakifanya hivi."
Akasema, "Je, mumewaona hawa mnaowaabudu nyinyi na wazee wenu waliotangulia? Bila shaka hao ni adui zangu ila Mola wa walimwengu wote, ambaye ameniumba na yeye ndio ananiongoza. Na ambaye ndiye anayenilisha na kuninywesha. Na ninapougua, yeye ndiye anayeniponesha. Na ambaye atanifisha kisha atanihuisha.Na ndiye ninayemtumaini kwamba atanisamehe makosa yangu siku ya malipo.

Mola wangu! nipe hukumu na uniunge pamoja na watendao mema. Na unijaalie katika warithi wa mabustani ya neema. Na umsamehe baba yangu, bila shaka yeye ni miongoni mwa waliopotea. Wala usinifedheheshe siku watakayofufuliwa, siku ambayo hayatafaa mali wala watoto.

Isipokuwa mwenye kuja kwa Mwenyezi Mungu na moyo safi, na pepo itasogezwa kwa wacha Mungu, na Jahanamu itadhihirishwa kwa wapotofu.

Na wataambiwa, "wapo wapi mliokuwa mkiwaabudu? Badala ya Mwenyezi Mungu! Je, wanaweza kukusaidieni au kujisaidia wenyewe? Basi watatupwa humo wao na maasi, na majeshi ya Ibilisi yote. Watasema, 'na hali ya kuwa wanagombana humo, 'Wallahi, kwa yakini tulikuwa katika upotofu ulio dhahiri. Tulipokuwa tukikufanyeni sawa na Mola wa walimwengu wote.'

Na hawatakupoteza ila wale waovu.
 'Basi hatuna waombezi wala rafiki halisi. Laiti kama tungelikuwa na marejeo tungekuwa waumini.'"

Bila shaka pana katika haya mazingatio, lakini wengi katika wao si wenye kuamini. Na kwa yakini Mola wako ndiye Mwenye nguvu, Mwenye rehema.

Sunday, June 21, 2015

Tumsifie Na Kumkumbuka Allah kila siku In'Shaa'llah

daily tasbih for ramduhn(english & arabic subtitles)

Aya ya Leo - Ayatul Kursi

Hii Aya waislamu tunashauriwa kuisoma kila siku, ukiisoma usiku, Allah anakuteulia mlinzi kukulinda usiku kucha na mabaya yote mpaka asubuhi. Na asubuhi pia ukiisoma, unapewa mlinzi wakukulinda mpaka usiku.

Mtume Muhammad(S.A.W) alisema, " Yule mwenye kuisoma hii aya baada ya kila sala, basi kifo ndo kinachomzuia yeye kuingia peponi."

Basi tujitahidi kuihifadhi hii aya.
 Ayatul Kursi - Miracles of Quran - Ustadh Nouman Ali Khan
 1. Mwenyezi Mungu - hapana mungu ila Yeye Aliye
hai.Msimamia mambo yote milele. 
2. Hashikwi na usingizi wala kulala. 
3.Ni vyake pekee vyote viliomo mbinguni na duniani. 
4.Ni nani huyo awezaye
kuombea mbele yake bila ya idhini yake? 
5.Anayajua yaliyo mbele yao na
yaliyo nyuma yao.
6. wala wao hawajui chochote katika vilio katika ujuzi
wake, ila kwa atakalo mwenyewe. 
7.Enzi yake imetanda mbinguni na duniani; 
8.Na wala haemewi na kuvilinda hivyo. 
9.Na Yeye ndiye aliye juu, na ndiye
Mkuu
(Qur'an 2:255)

Saturday, June 20, 2015

FUTARIIIII - MATUNDAAAA!!!!!

Ushanunua matunda ya Kufungulia?
 Mara ya mwisho umeenda sokoni mwenyewe kuchagua matunda lini?
Si mnajua lakini matunda hujenga mwili?
 Au teseme inasukuma vitu tumboni, wanasemaga magonjwa yote yanaanziaga kwenye utumbo.

Haya Futari njema wadau, ma fruit salad kwa wingi basi.


Friday, June 19, 2015

Aya za Leo - Hadithi ya Ibrahim(The story of Abraham)


Na Ibrahim pale alipo waambia watu wake: Muabuduni Mwenyezi Mungu, na mcheni Yeye. Hiyo ndiyo kheri yenu, ikiwa nyinyi mnajua.Hakika nyinyi mnaabudu masanamu badala ya Mwenyezi Mungu, na mnazua uzushi. Hakika hao mnao waabudu badala ya Mwenyezi Mungu hawakumilikiini riziki yoyote. Takeni riziki kwa Mwenyezi Mungu, na mumuabudu Yeye, na mumshukuru Yeye. Kwake Yeye ndio mtarudishwa. Basi haikuwa jawabu ya watu wake ila ni kusema: Muuweni au mchomeni moto! Mwenyezi Mungu akamwokoa na moto. Hakika katika hayo zipo Ishara kwa watu wanao amini. Na alisema: Hakika nyinyi mmeyashika masanamu badala ya Mwenyezi Mungu kwa mapenzi yaliyo baina yenu katika uhai wa duniani. Kisha Siku ya Kiyama mtakataana nyinyi kwa nyinyi, na mtalaaniana nyinyi kwa nyinyi. Na makaazi yenu ni Motoni. Wala hamtapata wa kukunusuruni. Lut'i akamuamini, na akasema: Mimi nahamia kwa Mola wangu Mlezi. Hakika Yeye ndiye Mwenye nguvu, Mwenye hikima. Na tulimtunukia (Ibrahim) Is-haq na Yaa'qub. Na tukajaalia katika dhuriya zake Unabii na Kitabu, na tukampa ujira wake katika dunia; naye hakika katika Akhera bila ya shaka ni katika watu wema.

And [We sent] Abraham, when he said to his people, "Worship Allah and fear Him. That is best for you, if you should know.You only worship, besides Allah , idols, and you produce a falsehood. Indeed, those you worship besides Allah do not possess for you [the power of] provision. So seek from Allah provision and worship Him and be grateful to Him. To Him you will be returned."And if you [people] deny [the message] - already nations before you have denied. And there is not upon the Messenger except [the duty of] clear notification.
And the answer of Abraham's people was not but that they said, "Kill him or burn him," but Allah saved him from the fire. Indeed in that are signs for a people who believe.And [Abraham] said, "You have only taken, other than Allah , idols as [a bond of] affection among you in worldly life. Then on the Day of Resurrection you will deny one another and curse one another, and your refuge will be the Fire, and you will not have any helpers."But Lut had faith in Him: He said: "I will leave home for the sake of my Lord: for He is Exalted in Might, and Wise."And We gave to Him Isaac and Jacob and placed in his descendants prophet-hood and scripture. And We gave him his reward in this world, and indeed, he is in the Hereafter among the righteous. 
(Qur'an 29:16-17,24-27)

Kweli kabisa bado tuna miminika kwenye msikiti wake alio ujenga yeye (Mwenyezi Mungu Aridhike nae) na mwanae nabii Ismail(A.S) kwaajili ya Mwenyezi Mungu.
Al-kaaba- Masjid Al-haram Makka

Jumaa Mubarak! 

Wednesday, June 17, 2015

Mwezi Umeonekana - Ramadhan Kareem 1436 (2015)

Alhamdullilah! Mwenyezi Mungu Katupa uzima kuona Mwezi wa Ramadhani, atupe uzime tuumalize salama.
Tuuanze na dua basi.

Mwenyezi Mungu akubali dua zetu sote.
Kesho Tunafunga In'shaa'llah.
We Start Fasting Tomorrow In'Shaa'llah.

Embrace Your Ramadhan Hunger


A couple of days ago, I had gone to bed without eating dinner as I had eaten a very heavy late lunch and was full the rest of the day and went to bed late. The next morning I overslept, for like a few hours over my usual time to wake up. This meant I had skipped my usual breakfast routine that happens a certain time of the day. So what happened to me, I woke up from my sleep with hunger pangs. I mean i felt extreme hunger, the kind where your stomach is growling and your body is shaking, and your about to bark at or eat the first thing you see. Well I quickly drank some fresh juice (After brushing my teeth of cause), which calmed me down instantly (Amazing!).

So this got me thinking, what if that day was Ramadhan, what would I have done? What would you have done?

For Me?  

NOTHING.


No Really there is nothing to do other than riding it out. I can count the number of times that I have experienced a hunger similar to this, its either in the beginning or near the end of Ramadhan,. It usually doesn't hit you in the morning, but rather sometime in the afternoon. The feeling is temporary, it doesn't last long, probably less than an hour or so, and mostly it happens if I didn't get in the proper nutrients and water the night before. The key here is to keep yourself occupied with something that will take your mind off the thought of food.

Some folks decide to sleep it out, although personally, this has only made it worse for me, you wake up hungrier than when you went to sleep. Just breathing through it in a daze while the mind wonders. Surfing the web, reading,watching tv, doing some light activity and even going to run errands if there is any energy left, is what has helped me in the past. All TV watching should be educational, motivational and God inspiring programs of cause.

Why Embrace it then?

Because its benefits are plenty. Your body is healing itself internally. Its not wasting its energy breaking down food in your digestive system, granted you didn't pig out the night before that is, and focuses its energy to repair damaged goods in your body. Allah has given us a great machine here, its up to us to allow it to do what it was designed to do. Your mind is more alert, notice how your mind wanders quickly to exotic cuisines that you haven't eaten in ages or seen on some TV Show, that's your brain working properly. The bottom line is you feel much lighter and focused, transfer that energy into doing positive things. Remember Allah, Read up on Islamic texts, do your 5 a day, and work on those projects that you were too lazy to finish. I bet you those great ideas will keep flowing.

To sum it up, you are at your best when hungry. So anticipate it, expect it,embrace it and humble yourself to it. This is a month of mercy and blessings, so maximize on it, by remembering and praying to him who created you, and be good and merciful to his creation. Remember the prophet said that the prayer of one who is fasting is never rejected.

 Ramadhan Kareem everyone!

Qaswida Kutoka Tanzania Leo - ARAFA ABDILLAH

JINA LANGU RAMADHANI(MY NAME IS RAMADHAN)
Translated Chorus:
My name is Ramadhan
My Visits are a Blessing
So You Muslims should fast
and be healthy

Monday, June 15, 2015

Friday, June 12, 2015

Aya ya Leo- Nuhu(Noah)

 
Na hakika tulimtuma Nuhu kwa watu wake, na akakaa nao miaka elfu kasoro miaka khamsini. Basi tufani liliwachukua, nao ni madhaalimu. 

And We certainly sent Noah to his people, and he remained among them a thousand years minus fifty years, and the flood seized them while they were wrongdoers. (Qur'an 29:1)

Friday, June 5, 2015

Aya za Leo - Wapotezaji(Those who lead Others Astray)

Na walio kufuru waliwaambia walio amini: Fuateni njia yetu, nasi tutayabeba makosa yenu. Wala wao hawatabeba katika makosa yao chochote kile. Hakika hao ni waongo.Na hapana shaka wataibeba mizigo yao na mizigo mingine pamoja na mizigo yao. Na kwa yakini wataulizwa Siku ya Kiyama juu ya waliyo kuwa wakiyazua.

And those who disbelieve say to those who believe, "Follow our way, and we will carry your sins." But they will not carry anything of their sins. Indeed, they are liars.But they will surely carry their [own] burdens and [other] burdens along with their burdens, and they will surely be questioned on the Day of Resurrection about what they used to invent. (Qur'an
29:12-13)
Ijumaa Njema Wadau!