Translate

Monday, May 6, 2013

Hatari; Bomu larushwa kanisani Arusha, mmoja afariki

Arusha.Mtu mmoja amefariki dunia na wengine 59 kujeruhiwa akiwamo Balozi wa Vatican na Mwakilishi wa Papa nchini Tanzania, Askofu Mkuu Francisco Montecillo Padilla jana asubuhi baada ya mtu asiyejulikana kurusha bomu wakati wa sherehe ya uzinduzi wa Jengo la Kanisa la Parokia ya Mtakatifu Joseph Mfanyakazi, Olasiti, Arusha.
Miongoni mwa majeruhi, imeelezwa kuwa wanne ni mahututi.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Arusha, Liberatus Sabas amelielezea kuwa tukio hilo kuwa ni la kigaidi hasa kutokana na kumlenga Balozi wa Papa nchini na kwamba mtu mmoja anashikiliwa akihusishwa nalo.
Wataalamu wa mabomu wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) wanachunguza aina ya bomu lililotupwa lakini uchunguzi wa awali unaonyesha lilikuwa limetengenezwa kienyeji.

Bofya hapa kwa habari zaidi kutoka gazeti la Mwananchi....

Ina lillahi wa Ina Illahi Rajiun. Kwa Mwenyezi Mungu ndio tunapotoka na ndio marejeo. Jamani hizi habari zinasikitisha sana, inakuwaje Binadamu hatuziheshimu tena sehemu za ibada, absolutely terrible. Nawaombea familia za marehemu na walioumia.

Update! 
Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Magesa Mulongo alisema watu tisa wamekamatwa hadi sasa.
Aliwataja baadhi yao kuwa ni Victor Ambrose na wengine aliowataja kwa jina mojamoja ni Joseph na David. Alisema wengine ni raia watatu wa Saudi Arabia, ambao walikuwa na wenyeji wao wawili na Watanzania wengine watatu. Wa Saudi waziri mkuu alisema bungeni wataachiwa. Soma Habari Zaidi Mwananchi



No comments:

Post a Comment